Huduma ya Majitaka
Mabwawa ya Kutibu Majitaka (Sewerage Treatment Ponds)
KUWASA ina Bwawa la Ustabilishaji wa Majitaka (Waste Stabilization Pond) lililopo eneo la Busoka lililopo ndani ya Manispaa ya Kahama, lenye mabwawa matano yanayofanya kazi kwa pamoja kwa mpangilio wa sambamba na mfululizo. Bwawa la kwanza ni la anaerobia, likifuatiwa na mabwawa mawili ya fakaltetivu yanayofanya kazi sambamba, na hatimaye mabwawa mawili ya kukomaza (maturation ponds) yanayofanya kazi kwa mfululizo. Ndani ya eneo la mabwawa hayo kuna mabwawa mawili ya tope (sludge ponds) kwa ajili ya kutibu maji yanayomwagwa kutoka kwenye Magari ya Majitaka. Kiasi cha wastani cha majitaka kinachoingia kila siku katika mabwawa yaliyopo ni mita za ujazo 6,443 kwa siku (6,443 m³/siku), ilhali uwezo wa kubuni (design flow) ni mita za ujazo 3,414 kwa siku (3,414 m³/siku). Aidha, KUWASA inaendelea kushughulikia mara kwa mara miundombinu ya maji taka, uendeshaji wa matibabu ya majitaka katika eneo hilo la Majitaka