Barua Pepe: info@kuwasa.go.tz  Simu (BURE): 0737 804 270 | 0737 804 271

 

Mamlaka Ya MajiSafi Na Usafi Wa Mazingira Kahama (KUWASA)

KUWASA ilianzishwa mnamo tarehe 21 Juni 2002 kwa sheria ya "water works Act cap 272" iliyofanyiwa marekebisho na sheria ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009.

KUWASA ipo katika daraja A. Hii inamaanisha kuwa Mamlaka ina wajibu wa kugharamia shughuli zote za kiutendaji na Maboresho ya Huduma.

Chanzo chetu cha Maji

Chanzo chetu cha maji ni Ziwa Victoria ambako maji yanasafirishwa kwa umbali wa kilomita 117 kwa mabomba.

Dhima Yetu

Kutoa huduma bora na endelevu za majisafi na usafi wa mazingira zinazokidhi vigezo kimataifa kwa bei nafuu.

Dira Yetu

Kuwa Mamlaka Bora katika kutoa huduma endelevu za Majisafi na Usafi wa Mazingira Nchini Tanzania.

Misingi Ya Utendaji Wetu

1. Kutimiza Dira na Dhima ya Mamlaka.
2. Kuboresha na Kukuza Ushirikiano na Kujituma
3. Uwazi
4. Ukweli
5. Uwajibikaji.
6. Wateja Kwanza
7. Watumishi ni Rasilimali namba moja ya Mamlaka
8. Kuwajibika kwa jamii inayotuzunguka
9. Wafanyakazi kuhimizwa kujifunza na kubadilishana maarifa

Malengo Yetu

1. Kuboresha Upatikanaji wa MajiSafi na Salama
2. Kuboresha makusanyo ya mwezi ya huduma ya Majisafi
3. Kuboresha utunzwaji wa Mazingira na Uhifadhi wa vyanzo vya maji
4. Kuboresha makusanyo ya mwezi ya huduma ya Majitaka
5. Kufanikisha kuboresha na kuongezwa kwa sheria ya MajiSafi na Usafi wa mazingira.

 

Menejimenti Yetu

Allen Marwa

(Mkurugenzi Mtendaji)

Missana Shija

(Meneja Biashara)

Allen Buyekwa

(Meneja Rasilimali Watu)

Renatus Nyamhanga

(Meneja Fedha)

Eng. Paul Luchanganya

(Meneja Ufundi)

Adam Mgongwa

(Mkuu wa Kitengo cha Ugavi)

John Mkama

(Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano)

David Charles

(Mkuu wa Kitengo cha Tehama)

Nuru Masoud

(Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani)

Fahamu Ankara Yako

Kila mwanzoni mwa mwezi Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama hutoa Ankara (Bili) za maji kwa wateja na kuzituma kwa njia ya meseji fupi (SMS). Ikiwa mteja hajatumiwa Ankara kwa mwezi husika, anaombwa kufika ofisini ili kuangalia taarifa zake na kulipia Ankara husika.

Usomaji wa Dira

Usomaji wa dira hufanyika kuanzia tarehe 15 hadi tarehe 23 ya kila mwezi. Zoezi hili hufanyika kwa watumishi wa Mamlaka kupita kwa wateja ili kuchukua taarifa mpya za dira. Uniti ambazo mteja wa huduma ya maji ambazo atakua ametumia hukokotelewa kwa kuchukua tofauti ya usomaji mpya kutoa usomaji wa zamani.
Wakati wa zoezi zoezi la kusoma dira watumishi wa Mamlaka huchukua taarifa zingine za dira kama dira kusoma tofauti au kama kuna uharibu wowote wa dira n.k.
Tunaomba wateja kuzingatia yafuatayo:-

  • Kutoa ushirikiano kwa wasomaji dira
  • Kwa wateja ambao dira zao zipo ndaji ya uzio, mtu awepo kwa kipindi hicho cha usomaji wa dira
  • Kuripoti tatizo lolote linalohusu dira kwa msomaji dira

 

Dira Yetu

Kuwa Mamlaka Bora katika kutoa huduma endelevu za Majisafi na Usafi wa Mazingira Nchini Tanzania.

Dhima Yetu

Kutoa huduma bora na endelevu za majisafi na usafi wa mazingira zinazokidhi vigezo kimataifa kwa bei nafuu.

Chanzo cha Maji

Chanzo chetu cha maji ni Ziwa Victoria ambako maji yanasafirishwa kwa umbali wa kilomita 117 kwa mabomba

 
Go to Top