Barua Pepe: info@kuwasa.go.tz  Simu (BURE): 0737 804 270 | 0737 804 271

Ufuatao ni utaratibu wa kuomba huduma ya Majisafi katika Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa mazingira Kahama.

Tunaomba waombaji wazingatie utaratibu huu na si vingenevyo.

Hatua za kufuata

1. Mteja atafanya maombi ya kuanganishiwa huduma ya maji kwa kujaza Fomu zinazopatikana Ofisi ya Mamlaka.
2. Fomu itasainiwa na Afisa Mtendaji/Mwenyekiti wa eneo husika.
3. Baada ya hapo mteja ataiwasilisha fomu Ofisi ya Mamlaka.
4. Wataalam wa Mamlaka watafanya ukaguzi (Survey) kwenye eneo/nyumba inayoombewa huduma ya maji na kutayarisha gharama zinazohitajika katika maunganisho hayo.
5. Gharama zote zinazohusika zitalipwa Mamlaka ya Maji na mteja atapewa risiti inayolingana na malipo aliyofanya.

Taarifa muhimu za mteja

  1. Mteja anapaswa kutoa majina yake kamili (majina matatu)
  2. Anwani ya eneo analotoka/ au mtaa anaoishi
  3. Hati ya nyumba au kiwanja anachokiombea huduma ya maji
  4. Namba ya simu
  5. Kitambulisho cha Taifa/Leseni ya udereva/kitambulisho cha Kupiga kura au Kitambulisho cha kazi.

Muda wa Huduma

  • Mteja akifanya malipo ya gharama za kuunganishiwa huduma atastahili kupatiwa huduma hiyo ndani ya siku saba kuanzia tarehe atakayokuwa amefanya malipo au siku kumi na nne eneo ambalo linahitaji kuendeleza bomba.
  • Iwapo kutakuwa na sababu zisizozuilika zitakazofanya mteja asipate huduma katika muda uliopangwa, Mamlaka itampa mteja taarifa rasmi.
  • Endapo mteja hatakua ameridhika na huduma atakayopewa ana haki ya kuwasilisha malalamiko yake kwa Afisa Uhusiano.
  • Mteja atatoa taarifa mara baada ya kupata huduma na ushauri kwa huduma aliyopewa.

TAHADHARI

Mamlaka haitahusika na mapatano au malipo yoyote yatakayofanywa nje ya utaratibu uliowekwa na Mamlaka.
Ukiwa na maulizo yoyote kuhusu maelezo haya Tafadhali fika Ofisini kwetu

Misingi ya utendaji wetu

1. Kutimiza Dira na Dhima ya Mamlaka.
2. Kuboresha na Kukuza Ushirikiano na Kujituma
3. Uwazi
4. Ukweli
5. Uwajibikaji.
6. Wateja Kwanza
7. Watumishi ni Rasilimali namba moja ya Mamlaka
8. Kuwajibika kwa jamii inayotuzunguka
9. Wafanyakazi kuhimizwa kujifunza na kubadilishana maarifa

 

Dira Yetu

Kuwa Mamlaka Bora katika kutoa huduma endelevu za Majisafi na Usafi wa Mazingira Nchini Tanzania.

Dhima Yetu

Kutoa huduma bora na endelevu za majisafi na usafi wa mazingira zinazokidhi vigezo kimataifa kwa bei nafuu.

Chanzo cha Maji

Chanzo chetu cha maji ni Ziwa Victoria ambako maji yanasafirishwa kwa umbali wa kilomita 117 kwa mabomba

 
Go to Top